Wanacheza – Unashinda Jiunge sasa
Mwanzo / / Jinsi Mkeka Wako Unavyofanya Kazi?

Parimatch imejizatiti kuhakikisha kuwa unatumia mfumo wetu kwa urahisi bila ya usumbufu wowote na kufurahia kucheza kwa utofauti, kuanzia unavyojisajili hadi unapoweka mkeka wako, tunataka ujisikie amani na furaha kucheza bila kukwama, ndiyo maana sisi ni kampuni namba 1 ya kubetia nchini Tanzania.

Likija suala la kuweka mikeka yako, utapata uhitaji wa kuzunguka kwenye mkeka wako, neno mkeka au jamvi ni la mtaani lakini watengeneza odds hupenda kuita “betting slip”. Ikionesha chaguzi zote ulizofanya na ni timu zipi au masoko yapi unataka kuyabetia, hamna tofauti na kikapu tu ukiwa sokoni.

Tunajua hii ni rahisi kwenye maduka ya nje ambapo unaingia unachagua timu zako kisha keshia anakupa mkeka wako na wewe unampa hela, Parimatch tumejizatiti kukupa urahisi zaidi kuliko wa madukani kwa kutumia mfumo wetu mtandaoni.

Na hii ndiyo sababu kubwa ya kuweka mkeka wetu kuwa rahisi na rafiki kwa watumiaji wetu wote, yaani unaingia kwenye mfumo wetu unachagua timu zako na masoko unayotaka kubetia kisha unabetia bila usumbufu.

Kama utapata shida kwenye uwekaji wa mkeka wako au kukwama kwa namna yoyote ile, tumekuandalia mnkala hii fupi ya kukusaidia kujua inafanyaje kazi na itakuwaje msaada kwa upande wako.

Mkeka ni Nini?

Kwenye app ya michezo ya kubashiri ya Parimatch, tunatumia neno la kuwakilisha mkeka wa kielektoniki kama “betslip” kipengele hiki cha tovuti au app yetu kinaonesha taarifa zote kuhusu mkeka uliyoubetia na Parimatch.

Mkeka au tuseme betslip itakupa taarifa zote za mkeka uliyouweka, itakuonesha pia timu zote ulizozipa ushindi au kuzinyima na ukubwa wa odds ulizonazo pamoja na thamani ya mkeka wako kulingana na dau lako ukizangatia masoko uliyoyacheza, mfano 1X2, halftime/fulltime, handicap na mengine mengi uliyoyaweka kwenye mkeka wako.

Tuchukile mfano kwenye picha hii, hapa unaweza kuona mkeka wa kwanza ni 1X2, kubetia kwa Newcastle UTD U-23 kushinda. Mkeka wa pili ni wa halftime/fulltime, ukiwa na ubashiri wa sare kipindi cha kwanza na kushinda mchezo mzima kwa Leicester. Mkeka wa mwisho ni handicap ukionesha Getafe watashinda kwa zaidi ya magoli mawili.

Multibet on Parimatch Tanzania

Mkeka wako utakuonesha odds kwa kila timu upande wa kulia, hii husaidia kufuatilia odds zako na kupiga mahesabu na kujua mabadiliko ya odds hasa ukiwa unabetia live.

Mkeka wako pia una sehemu ya kuonesha idadi ya matukio au mechi zilizopo kwenye jamvi lako pia unaweza kuona kiwango cha kodi ulichokatwa na jumla ya kiwango cha hela utakachoshinda baada ya kukatwa kodi.

Mkeka wako au kitaalamu zaidi betslip utakuwezesha kuhifadhi taarifa zote muhimu unazohitaji kuanza nazo na idadi ya timu, ukubwa wa odds, dau uliloweka, kodi pamoja na pesa zako zote ulizoweka na unazotegemea kushinda.

Mkeka Unafanyaje Kazi?

Kitufe cha mkeka kimewekwa kwenye kona ya kushoto kwenye app yako ya Parimatch au kwenye tovuti ukishamaliza kuchagua timu zako unakibofya tu ili kukamilisha mkeka wako. Kitufe hiki kitakuongoza kwenye sehemu unayotakiwa kukamilisha mkeka wako.

Kama tulivyokwishakueleza awali kipengele hiki kinakupa fursa ya kukamilisha mikeka yako na kukupa uhifadhi wa kumbukumbu zako muhimu za mkeka wako kwa siku hiyo.

Japo mkeka hauna kazi hizo tu, hii ndiyo sehemu ya kujua kiwango cha pesa unachotumia na kushinda ili ujue kama unapata faida au lah na kuweza kuboresha mbinu zako zaidi.

Single bets kwenye mkeka wako

Kwanza kabisa, kwa wale wateja wanaobetia kwenye mechi moja au tukio moja kwa mara moja, betslip inakupa fursa ya kuhakikisha kama chaguzi yako ipo sahihi kabla ya kuulipia mkeka wako, vilevile kupitia uwepo wa betslip unaweza kuchagua kiwango cha chini kabisa cha kubetia ambacho kwentu ni TZs 300 au unaweza kuchagua dau kubwa zaidi unalotaka, vilevile unaweza kujua utashinda shillingi ngapi kabla na baada ya kodi.

Kwa wale wanaotaka kucheza kwenye mechi nyingi zaidi, unaweza tu kuchagua kuhamia kwenye sehemu nyingine ya betslip yako inayoitwa Parlay.

Parlay bets kwenye mkeka wako

Eneo la mkeka au betslip linawawezesha watumiaji wa app ya Parimatch kuweka parlay bets kwa kubofya kwenye kitufe kilichoandikwa “Parlay” kushoto juu ya mkeka wako. Kwa kubofya hivi mkeka wako utaidhinishwa kama Parlay.

Je, nini maana ya Parlay bets? Kwa kubofya kitufe cha parlay kwenye mkeka wako unabadilisha kuwa accumulator. Hii inamaanisha chaguzi zako zote zitaungnaishwa kwenye mkeka mmoja na utakuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda hela nyinyi zaidi. Kwenye parlay utahitaji tmu zako zote zishinde ili uweze kulipwa, tuseme ukiweka mkeka wa mchi zako 6, zikashinda tano bado hautaweza kulipwa. Kwa taarifa zaidi tembelea jinsi ya kucheza parlay bets.

Ili uweze kucheza parlay bets inakubidi uweze kuchagua mkeka zaidi ya mmoja ukicheza na Parimatch, utaona mikeka yako imewekwa chini ya “parlay”.

Nini maana ya “Add to Betslip”?

Ukiwa unabeti na Parimatch tunataka ujisikie huru na kufurahia safari nzima ya kucheza na kwa urahisi wa hali ya juu, ndiyo maana tunapunguza idadi ya hatua unazotakiwa kuzifuata ili kuweka mkeka wako kwenye timu zako pendwa.

Ukiwa unabeti na Parimatch, unahitaji kuongeza gemu kwenye betslip yako ili mfumo wetu uweze kurekodi chaguzi zako kwa usahihi, hivyo unavyosikia add to betslip ni pale ambapo unatakiwa kuongeza chaguzi zako kwenye mkeka wako ili ziweze kuongezwa kwenye jumla ya timu zote unazotaka kuzibetia. Ukishachagua add to betslip baadaye unaweza kwenda kuchagua kama unataka kucheza parlay au system kwenye sehemu ya slip.

Kwa bahati nzuri, tukiwa tunazidi kuboresha na kurahisisha mfumo wa kubeti kwa wateja wetu wote, ni rahisi sana kuchagua kuongezea kwenye mkeka au add to betslip, kuleta urahisi kwa wateja wetu, app yenyewe itakuonesha unapotakiwa kubofya ili kuongeza chaguzi zako kwenye mkeka wako.

Kama unavyoona, bokis lenyewe linakuwa ni jeusi kuonesha chaguzi zote ulizozifanya, utaona chaguzi zako kwenye matukio kwenye mkeka wako.

Jinsi ya Kuangalia Mkeka Wako na Parimatch

Parimatch tunajivunia kwa kuwa na moja kati ya app zenye ubora wa hali ya juu kuanzia kwenye mfumo mzima hadi muonekano unaoleta urahisi kwa watumiaji wetu, tunajaribu kuhakikisha mikeka yote inawekwa kwa usahihi na mteja hakosei kuweka mkeka wake kutokana na makosa ya kiufundi, ndiyo maana ni rahisi kuangalia mkeka wako.

Kwanza kabisa, kwenye chaguzi za michezo boksi hubadilika rangi na kuwa jeusi kwa kila chaguzi unayoifanya ili kukujulisha ulichochagua kupunguza uwezekano wowote wa kufanya makosa, unaweza kuchagua betslip kwa kubofya kitufe chenye alama ya mkeka wako kulia kwenye tovuti au app yako ya Parimatch.

Kwanini unahitaji kuangalia mkeka wako?

Ukiwa unabetia ni muhimu kujua umechagua vitu sahihi ikiwa ni pamoja na timu sahihi ili uweze kubetia kwenye matokeo sahihi unayoamini yatatokea, pesa nyingi zinaweza kupotea ukikosea kuweka mikeka, ukikosea tu kuchagua timu moja inaweza kukuvurugia mkeka wako wote.

Kuangalia mkeka wako kunamaanisha kuingia kwenye orodha ya mikeka yako na kuangalia kila kitu kipo sawa, timu zipo kwa usahihi, masoko unayoyataka umeyachagua na kujua kiwango gani cha fedha unachoweka kwenye mkeka huo.

Kabla ya kubofya betslip au kumalizia kuweka mikeka yako lazima uwe muangalifu kama umechagua kubetia kwa mfumo wa system au parlay, kitu cha mwisho unachotaka kukosea ni mfumo unaotaka kubetia na kutokutimiza malengo yako, ukichagua system badala ya parlay na ukashinda utashangaa umeshinda pesa kidogo sana.

Jinsi ya Kutumia Mfumo wa Mkeka na Parimatch

Ukiwa unaweka mkeka wako na Parimatch, ni muhimu kuzoea jinsi mfumo wetu wa mkeka unavyofanya kazi au kwa jina lingine betslip ukiwa unakamilisha mkeka wako, kwa bahati nzuri ni rahisi sana kuanza, fuata tu hatua zifuatazo:

  1. Jisajili (Ingia) kwenye website au app;
  2. Weka Pesa;
  3. Chagua mechi zako;
  4. Chagua aina ya mikeka unayotaka kuicheza;
  5. Chagua matokeo ya timu gani unaamini itashinda;
  6. Rudia hatua 3-5 kuongeza idadi ya timu kwenye mkeka wako;
  7. Nenda kwenye mkeka;
  8. Chagua kama unataka kucheza single au parlay bets;
  9. Weka dau unalotaka kuweka kwa umakini;
  10. Weka mkeka wako.

Soma Zaidi:

Mwisho

Kama unavyoona, ni rahisi sana kucheza na kushinda na Parimatch, mfumo mzima umetengenezwa kukuwezesha kufikia malengo yako ya kubetia na kushinda kiufundi na sisi yakamilike, hivyo siyo kitu cha kushangaza kutambulika kwetu kama moja ya kampuni bora zaidi za kubetia nchini, kuanzia hapo chagua singles, parlay, au systems bets.

Kumbuka kwamba mkeka wako ni kumbukumbu ya mikeka yako yote, kwa kutengeneza mkeka wako na Parimatch, unajiwekeka rekodi ya mikeka yako yote ili uweze kujua mwenendo wako mzima, hivyo ni rahisi hata kujua kama unahitaji kuboresha mbinu zako au lah.

Maswali ya Mara kwa Mara

Je, mikeka huwa inalipwa vipi?

Mikeka hulipwa kwa kukokotoa dau lililozidishwa na uwezekano wa desimali. Kwa mfano ukishinda TSh. 20,000 na odds 2.0, dau linalipa Tsh. 40,000. Kadri idadi ya odds inavyoongezeka kunakuwa na uwezekano mdogo wa matokeo kutokea. Hii inaelezea ni kwanini malipo ni ya juu.

Je, unajazaje mkeka?

Weka mikeka yako kwenye michezo yako, na mfumo utaupanga mkeka moja kwa moja. Unaweza kuangalia maendeleo ya mkeka uliobeti kila wakati kwenye mkeka wako husika. Unaweza kuupata kwenye upande wa kushoto wa dashibodi ya akaunti yako au sehemu ya chini ya dashibodi yako kama unatumia programu ya Parimatch.

Inamaanisha nini kuongeza mechi kwenye mkeka?

Mkeka ni hati ya elektroniki ya kubetia inayoonesha dau la wote waliobeti. Mkeka wenye dau hukuonesha taarifa zote kuhusu mikeka yako ya Parimatch.

Je, unahitaji kuwa wa kwanza kupata taarifa mbalimbali?

Subscription was successfully completed.